Saturday, 12 October 2013

kada wa ccm afariki dunia leo.



source, ccm

Meya mstaafu ashinda kesi ya mauaji

na Sitta Tumma, Mwanza

VILIO vya furaha jana vilitawala katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza baada ya aliyekuwa Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Leonard Bihondo na wenzake watatu kuachiwa huru katika kesi ya mauaji ya aliyekuwa Katibu wa CCM Kata ya Isamilo, Bahati Stephan iliyokuwa ikiwakabili.
Akisoma hukumu hiyo ya shauri namba 79 la mwaka 2011, Jaji Aisheri Sumari alisema kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri umeshindwa kumtia hatiani mshitakiwa namba moja katika kesi hiyo, Jumanne Oscar ambaye alituhumiwa kutekeleza mauaji hayo kwa kumchoma Bahati kisu katika ziwa lake la kushoto.
Akisoma maelezo ya shahidi namba 16 na 18 ambao walikuwa ni askari polisi waliokabidhiana mtuhumiwa namba moja, alisema kuwa ushahidi wao ulikuwa na mkanganyiko hivyo kutoa faida kwa washitakiwa.
Jaji Sumari alisema kwa maelezo yao, shahidi namba 16 anasema kuwa alipelekwa mahabusu na shahidi namba 18 kumchukua mshitakiwa namba moja, kisha kmpeleka kwa RCO Muna kuchukuliwa maelezo.
Aliongeza kuwa shahidi namba 18 katika ushahidi wake alisema kuwa tangu alipomkabidhisha mtuhumiwa kwa OCD siku ya tukio, hajawahi kurudi wa kushughulika na kesi hiyo hadi alipokwenda kutoa ushahidi mahakamani.
“Mkanganyiko huo ulitakiwa kuondolewa na Malingumu ambaye mpaka sasa ni askari, lakini upande wa Jamhuri wameshindwa kushughulika na hilo, hivyo kushindwa kuamini maelezo ya ushahidi,” alisema.
Jaji Sumari alisema kuwa pande wa mashitaka haukutaka Malingumu kufika mahakamani kuthibitisha mtuhumiwa aliyekabidhiwa na shahidi namba 18 (Sostenas) kama ndiye mshitakiwa namba moja.
Alisema kuwa uwezekano wa kuwachanganya washitakiwa ni mkubwa kutokana na ushahidi uliotolewa na shahidi namba 16 na 18, kwa sababu kama mshitakiwa namba moja ndiye aliyekamatwa ziwani, haoni kwanini awe na majeraha wakati shahidi namba 7 na namba 2 walimkabidhi mtuhumiwa kwa askari bila majeraha yoyote.
Kufuatia maelezo hayo, Jaji Sumari alisema kuwa kuna mkanganyiko mkubwa upande wa mashahidi wa Jamhuri juu ya mtu aliyechukuliwa na polisi na mtuhumiwa aliyetolewa ziwani.
“Hapa kuna maswali mengi ya kujiuliza, kwanini upande wa Jamhuri hawakuita gwaride la utambuzi kwa sababu wananchi ndio waliomkamata mtuhumiwa ziwani na kumkabidhi kwa askari wakati kesi hiyo imechukua muda mrefu?” alihoji.
Alisema kuwa anakubaliana na hoja za wakili wa mshitakiwa wa kwanza, Stephan Magoiga kuwa ushahidi unaotolewa hapo ni utambuzi wa mahakamani na si eneo la tukio ambapo mahakama haiwezi kumtia hatiani mshitakiwa huyo.
Kuhusu upande wa utetezi wa washitakiwa, Jaji Sumari alisema kuwa mtuhumiwa namba moja ambaye alikuwa na kesi ya kujibu aliuchambua vizuri ushahidi uliotolewa na shahidi namba 16 na 18 na kudai kuwa umeonyesha wazi mkanganyiko kutokana na vielelezo vya nguo ambavyo alikuwa amevaa.
Alisema kuwa mashahidi hao walimtambua kwa suruali aliyokuwa amevaa aina ya jinzi ambapo kielelezo kilichofikishwa mahakamani ni cha suruali ya khaki ambayo ilikuwa na damu.
Kutokana na maelezo hayo, Jaji Sumari alisema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri kuwa hauwezi kuwatia hatiani washitakiwa wote wanne, hivyo akawaachia huru.

Source; Tanzania daima

ZITO AFICHUA NJAMA NZITO


ZITTO AFICHUA NJAMA CHAFU
na Abdallah Khamis, Bukene

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe amesema kuna njama inayofanywa na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutaka mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya usiishe ili wajiongezee muda hadi mwaka 2017.
Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema kuwa lengo la wabunge hao ni kutaka muda wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 usogezwe mbele hadi 2017 ili waendelee kukaa madarakani.
Alisema kuwa CHADEMA haitakubali uvunjwaji wa aina yoyote wa katiba, na hivyo kumtahadharisha Rais Jakaya Kikwete kutothubutu kukubaliana na fitna hizo.
Madai ya Zitto yaliwahi pia kutolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alisema kuwa CCM wanataka kukwamisha mchakato wa katiba makusudi ili kutengeneza sababu ya kuongeza muda wa Rais Kikwete kubaki madarakani kwa miaka miwili zaidi.
Prof. Lipumba alisema kuwa hoja ambayo CCM wanataka kuitumia kukwamisha mchakato huo, ni muundo wa serikali ambapo dakika za mwisho wanataka kukubali serikali tatu kisha watumie kisingizio cha uundwaji wa taifa la Tanganyika kuchelewesha katiba mpya.
Akihutubia mikutano mbalimbali ya hadhara katika Jimbo la Bukene mkoani hapa, ukiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya ujenzi wa chama katika Kanda ya Magharibi jana, Zitto alisema hata vurugu zilizotokea bungeni hivi karibuni na Naibu Spika Job Ndugai, kuruhusu askari waingie ndani ya Bunge kuwakamata na kuwapiga wabunge wa upinzani, ilikuwa ni sehemu ya mpango huo wa kutaka kusogezwa mbele kwa muda wa wabunge kutoka madarakani.
Zitto alifafanua kuwa hoja inayojengwa na wabunge hao ambao wameshaanza kuipenyeza kwa ajili ya kumfikia Rais Kikwete, ni kwamba kama katiba mpya itapatikana kwa wakati huu, muda wa kujiandaa na uchaguzi wa mwaka 2015 utakuwa hautoshi.
“Hawa ni wabunge waroho wa madaraka, hawajafanya jambo lolote jema katika majimbo yao, na sasa wanajua hawawezi kurudi ndiyo maana wanataka muda usogezwe na wao waendelee kulipwa mshahara na posho.
“Sisi CHADEMA tunasema hilo hapana, hatuwezi kukubali uchaguzi usogezwe kwa miaka miwili, na namuonya Rais Kikwete asithubutu kuingia katika mkenge huo unaowahusisha baadhi ya mawaziri,” alisema.
Aliongeza kuwa wananchi waliwachagua wabunge wao kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano, na kwamba kuwe na katiba mpya au isiwepo ni muhimu uchaguzi kufanyika ili wale walioshindwa kuwajibika wakae pembeni.
Zitto alisema CHADEMA inatoa kauli hiyo ili wananchi wajue mkakati huo, na washiriki kuupigia kelele, kwa kile alichoeleza kuwa mipango hiyo imeshaanza jijini Dar es Salaam na Dodoma.
Kwa mujibu wa Zitto, baadhi ya mawaziri wanataka kutumia nafasi ya kuwa karibu na rais ili kumshawishi akubali mkakati huo, kwa kumueleza kuwa hali hiyo itamjengea heshima na kumbukumbu ya kuiachia nchi katiba iliyo bora.
Avunja ngome ya CCM
Katika hatua nyingine, Zitto ameitikisa ngome ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi.
Dalili ya ngome hiyo kutikiswa ilianza kuonekana mapema wiki hii wakati viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Uyui walipokuwa wakifanya maandalizi ya mkutano katika Kata ya Mabama, ambako ni nyumbani kwa kigogo huyo.
Baada ya kutangazwa kuwapo kwa mkutano wa CHADEMA katika kata hiyo, gazeti hili lilishuhudia jitihada mbalimbali za viongozi wa CCM zikifanyika, ikiwemo kuweka bendera mpya kila baada ya nyumba mbili, huku zile nyumba za wakazi wasiokuwa wafuasi wa chama hicho, zikiwekwa barabarani.
Baadhi ya wakazi wa kata hiyo na maeneo mengine ya jirani ambao walijitokeza kumsikiliza Zitto, walieleza kuwa baadhi ya nyumba zilizowekwa bendera wakazi wake walitishiwa kufanyiwa hujuma kupitia ofisi ya mtendaji wa kata hiyo endapo wangekataa.
“Unaona bendera zote ni mpya, hapa tumewachoka, na sasa wanatumia vitisho kutaka kuweka bendera zao kwenye nyumba zetu,” alisema mmoja wa wakazi hao ambaye hakutaka kutajwa jina.
Hata hivyo, mkutano wa Zitto nusura uingie dosari baada ya msafara wake kuchelewa kufika katika Kata ya Mabama, kisha mtu aliyejitambulisha kama ofisa mtendaji wa kata hiyo, kuwataka wananchi watawanyike kutoka katika uwanja wa mkutano.
Lakini wananchi hao hawakukubaliana na agizo hilo na kuahidi kumsubiri Zitto ambaye aliwasili katika eneo la mkutano saa 12:47 jioni na kuwahutubia hadi saa moja na robo usiku.
Kabla ya kuhutubia mkutano huo, Zitto aligawa kadi kwa wanachama wapya waliotoka CCM na kuwataka wasiogope vitisho vyovyote vinavyofanywa na viongozi wa chama hicho.
Alisema CCM imeua njia ya reli iliyokuwa ikiwasaidia wakazi wa Mabama kufanya shughuli za kila siku za kujipatia kipato.
Hata hivyo, Wakasuvi alikanusha chama chake kujihusisha na vitendo vya kuwatisha wananchi, akisema kuwa wao wanatumia nguvu ya hoja.

SOURCE: Tanzania Daima.


YES IS NOT

By all means, marry. If you get a good wife, you'll become happy; if you get a bad one, you'll become a philosopher.

Tuesday, 1 October 2013

 PCCB YAMWAGA NAFASI ZAIDI YA 500 ZA KAZI (AJIRA ) KWA VIJANA WA FANI MBALIMBALI , DEADLINE NI OCTOBER 21/ 2013...SOMA HAPA USIPITWE!!!

1. Investigation Officers(214post)
Direct Entarants(From Colleges/Universities)
Applicants should posses thre yeas advanced diploma or undergraduate degree from recognized higher learning institutions in anya of the following fields:Quantity Survey,Accountancy,Human Resources Management,Law,Procurement,Journalism,Information Technology,Highway Engineering,Building Constructions,Electrical Engineering,Lamd management and Evaluation and Forensic Knowledge


Required Qualification:
-All applicants must be citizens of Tanzania not above 35 years old
-Applicants should have a minimum pass of lower second class
-Applicants must attach their detailed relevant certified copies of academic certificates:
    -Degree/Advanced Diploma Transcript and certificates
    -Form four and form six National Examination certificates
    -Standard seven completion certificate
    -Professional certificates from respective boards(added advantage)
    -One recent passport size picture and birth certificate
    -Postgraduate Degree Transcripts and certicates(added advantage)
-Applicant should have good working knowledge of ICT(with related software,phone,fax,email,the internet and computer application eg MS Office)
-Applicants in th law field must have postgraduate diploma in legal practice(Law School oof Tanzania graduate) or passed the Bar exam and enrolled in the role of advocates.


Applicants in the Information Technology field must posses the following qualifications:
-Bachelor of science(BSc) in computer science/computer engineering/Electronics/Information Technology
-Certificate in A+ or Microsoft Certified Technology Specialist(MCTS) is an added advantage
-Data mining

2.0 Assistant Investigators(180 posts)
2.1 Personal Secretaries(8 Posts)
Qualifications:
-Applicants should posses Secondary School Certificates with passess in English and Kiswhili
-Diploma in Secretarial studies
-Short Hand 80 Wpm
-Computer literacy at least windows,microsoft office, internet,e-mail,microsoft publisher


Duties and Responsibilities:
-Performs Secretarial and Office management duties
-Keep custody of records,files,register and computer,e-mail,massages and ensure ther are properly channeled to respective destination
-Assist in coordinating secretarial function with other depatments
-Deal with all appointment Schedules for relevant officers
-Perform any other duties as may be assigned

2.2 Assistant Acountant(10 post)
Qualifications:
-Applicants should posses secondary school certificate with pass in english and kiswahili
-Applicants should also posses certicate in Accounting Technician 2(ATEC 2-NBAA) or Diploma in accountancy from recognized Institute
Duties and Responsibilities
-To issue cheque and prepare cheque book returns
-To prepare Unused Recipts Returns
-To maintain petty cash
-To prepare monthly statements or outstanding imprest
-To prepare imprest payment vouchers
-To prepare imprest journal vouchers
-To ensure all filing is done in timely and accurate manner


2.3 Watchmen(95 Posts)
Qualifications:
-Applicants should have completed form four or six and undergone voluntary Natinal Service Training
-Training in security guard duties,local military and fire fighting techniques is an added advantage
Duties and Responsibilities:
-To patrol arround the premises and buildings during the night according to the laid down procedure
-To secure security for buliding and other PCCB properties
-To check all gate passes at the main gate to ascertain that vehicles and other Properties,going out of the premises of the PCCB are authorized as shown in the gate pass and that the gate passes are authentic
-To check all visitors,vehicles and property coming into the premises of the PCCB through the main gate whether it is legitimate in relation to accompanying documentation
-To ensure that hazardous materials are not smuggled into premises
-To write a duty reports and Submit them to higher authorities
-To carry out any other tasks related to the above mentionedand functions of the PCCB that she/he may be assigned by the Head of Administration
-Any other duties that may be assigned by his/her superior

2.4 Drivers(25 Posts)
Qualification:
-Form four or six leavers with a class C driving Licence(more than three year driving experience)
-Applicants should also posses Certificate of Competence from the National Institute of Transport(NIT) Dar es salaam or Institute of Technology(DIT) or Vocatinal Education Training Authority(VETA)
Duties and Responsibilities:
-To manage and drive vehicles they are assigned in accordance with traffic regulations:
-To inspect the vehicle before and after a journey to ensure that it is in good condition
-To fill in the Log Books and ensure that the vehicle is used for authorized purpose only
-To advise the Bureau on repair and maintenance of the vehicle

2.5 Office Attendants(38 posts)
Qualifications:
-Applicants should have completed and passed form four or form six.
-Certificate or diploma in Record management,front office hospitality,customercare and other related fields is added advantage
Duties and Responsibilities:
-To clean the premises and buildings of the bureau
-Take massages and mail from one place to another within the premises or outside
-The office attendant is responsible to the office suprvisor and responsible fro taking proper custody of property of the bureau
-Swicth off all rights,air conditions,fans and any other electrical equipment that ought to cease operating after working hours

2.6 Technicians(4 Post)
Qualificatons:
-Possesion of a Secondary School Education Certificate
-Possesion of a FTC or Ordinary Diploma in a related field
Duties and Responsibilities:
-Undertake minor works repair and other facilities
-Conducting regular inspection of the working tolls and facilities
-Determining maintenance and repirs required(fax machine,photocopy,printers,electricity,air conditins,water and sewage system)
Basic attributes for above positions:
-Self Motivated
-Role Model
-Integrity and Profesional Ethics
-Strong Intepersonal Skills
Remuneration:
According to the government Circular
Mode of application:
-Interested candidates should send their applications enclosingtheir current CV's,copies of relevant academic certificates,having reliable physical address,posta address,email,telephone numbers,certified photocopies of birth certificate and recent passport size photograph
-Applicatants must submit three names of reliable referees
-Indicate in an envelope clearly a post you are applying for marked as "Application for the post of...."(insert post) and send your application letter to the following address:
The Director General,
Prevention and Combating of Corruption Bureau,
P.o.box 4865
Dar es salaam
Deadline of application:21st October,2013

"HAND DELIVERY IS NOT ACCEPTABLE"

 
Source:Dailynews 30th September,2013.