Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage akiwaonyesha waandishi wa habari
(hawapo pichani) katiba ya Simba katika mkutano alioufanya jana Jumapili
kuhusu kusimamishwa kwake. Mkutano huo ulifanyika makao makuu ya klabu
hiyo, Barabara ya Msimbazi, Dar es Salaam. Picha na Michael Matemanga.
Na Sosthenes Nyoni, Mwananchi
Posted Jumatatu,Novemba25 2013 saa 14:27 PM
Posted Jumatatu,Novemba25 2013 saa 14:27 PM
Kwa ufupi
Awali, Rais wa TFF, Jamal Malinzi akizungumza
na Wanahabari alimtaka Rage aitishe mkutano mkuu wa mabadiliko ya katiba
ndani ya siku 14 kuanzia Novemba 23.
Rage amemteua Wambura kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba.
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa
Simba, Ismail Rage amepinga agizo la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
linalomtaka aitishe mkutano wa mabadiliko ya katiba ndani ya siku 14 na
kusema endapo msimamo huo utasisitizwa basi atajiuzulu.
Awali, Rais wa TFF, Jamal Malinzi akizungumza na
Wanahabari alimtaka Rage aitishe mkutano mkuu wa mabadiliko ya katiba
ndani ya siku 14 kuanzia Novemba 23.
“Kutokana na Mgogoro uliopo Simba hivi sasa,
kamati ya utendaji ya TFF inamwagiza mwenyekiti wa Simba, Aden Rage
kuitisha mkutano mkuu wa dharura ndani ya siku 14 kuanzia sasa.
“Uamuzi huu umefanywa kwa kuzingatia ibara ya 1(6)
ya katiba ya Simba inayosema Simba Sports Klabu ni mwanachama wa TFF,
itaheshimu katiba, kanuni, maagizo na uamuzi wa TFF,” alisema Malinzi.
Lakini jana mwenyekiti wa Simba, Rage akizungumzia
agizo hilo la TFF alisema hawezi kuitisha mkutano huo kwa shinikizo la
shirikisho hilo.
“Katiba ya TFF ibara 31(1-5) inasema mjumbe wa
kamati ya utendaji atakosa sifa kama atakosa mambo manne, ataandika
barua kujiuzulu, haudhurii mikutano minne iliyoitishwa na mwenyekiti
halali, kama atakuwa mgonjwa amelala kitandani miezi 12 mgonjwa na
amekutwa na kosa la jinai,” alisema Rage.
Alisema,” nimesikitishwa na agizo la TFF kunitaka
niitishe mkutano ndani ya siku 14, wamenukuu ibara ya 1(6), Simba
Sports Club ni mwanachama wa TFF, nitaheshimu katiba, kanuni, maagizo na
uamuzi wa TFF, hatuwezi kuheshimu kuvunja katiba ya TFF, mimi naambiwa
nivunje katiba ya TFF naambiwa nivunje katiba ya Simba.”
“Tena wamekwenda mbali wananitaka niitishe mkutano
ndani ya siku 14 sijui wameitoa wapi, haipo kwenye katiba ya TFF wala
Simba, mimi msimamo wangu kama mwenyekiti wa Simba siitishi mkutano
nalindwa na katiba,” alisema Rage.
Akizungumzia kamati ya utendaji iliyoketi na
kumsimamisha, Rage alisema ilikuwa batili kutokana na kuongozwa na mtu
ambaye hatambuliki katika katiba ya klabu yake ya Simba.
“Kamati ya utendaji ya Simba inakamilika kwa kuwa
na mwenyekiti, makamu mwenyekiti na wajumbe saba waliochaguliwa katika
uchaguzi halali, hakuna sehemu inayomtaja kaimu mwenyekiti au umewahi
kuona wapi mtu ana kaimu na kukaimu, huyo Itangire si amewekwa tu pale,
alichaguliwa na nani?” Alihoji Rage. Alijitapa kwa kusema hatua yake ya
kwenda kuzunguza makao makuu ya klabu yake imedhihirisha yeye ndiye
mwanaume wa kweli na aliwaponda wapinzani wake kwamba ni waoga kutokana
na kumjadili mafichoni.
“Siku zote ukitaka kupindua nchi unaanza kuteka Ikulu, mimi ndiyo mwanaume wa kweli siyo hao wanaoongelea huko uchochoroni huo si uoga?” alijigamba Rage.
Katika hatua nyingine, Rage amemteua Michael Wambura kuwa mjumbe wa
kamati ya utendaji ya Simba na kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Rahma Al
Kharoosi aliyejizulu kutokana na kutingwa na majukumu.
SOURSE: MWANANCHI.
No comments:
Post a Comment