Na Mwandishi Wetu
MJUMBE wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini Dk. Sendongo Mvungi amefariki dunia.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba Assaa Rashid jana jioni alisema Dk.Mvungi alifariki saa 8:30
mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.
“Kwa masikitiko makubwa,Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe
wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya
Milpark iliyopo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini amefariki
dunia leo(jana),”alisema.
Rashid katika taarifa yake fupi ya awali alisema :”Taratibu za
kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini
kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa kesho(leo)”.
Marehemu Dk. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, mwaka
huu kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea
Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa
nyumbani kwake Kibamba, jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya
kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.
Katika taarifa hiyo, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na
familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dk. Mvungi katika
kuomboleza msiba huo.
source: jambo leo.
No comments:
Post a Comment