Friday, 15 November 2013

Timu 11, zitakazofuzu kwa Kombe la Dunia zitaanza kupambana baada ya wiki wakati wa michezo ya mtoano wenye timu 32.


Paris, Ufaransa. Vita ya kusaka timu nne za Ulaya za mwisho kufuzu kwa Kombe la Dunia 2014 inaanza leo kwa Ufaransa na Ureno kupigania heshima ya kuugana na vigogo wenzao Hispania na Ujerumani waliotangulia Brazil.
Ureno inayoongozwa na Cristiano Ronaldo watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Sweden, ambayo itakuwa nchini ya Zlatan Ibrahimovic.
Mabingwa wa zamani Ufaransa wenyewe watakuwa ugenini Kiev kuivaa Ukraine wana matumaini kidogo ya kufuzu, lakini si kwa utata kama ule wa 2010 wakati waliposubiri hadi bao la mkono la Thierry Henry liliitoa Ireland.
Mechi nyingine itawakutanisha Ugiriki dhidi ya Romania, huku timu ndogo ya Iceland itakuwa ikisaka nafasi ya kuwa taifa dogo kufuzu kwa mara ya kwanza kucheza fainali hizo wakati watakapoikabili Croatia.
Kocha wa Ureno, Paulo Bento, ambayo aliiongoza timu hiyo kufuzu kwenye nusu fainali ya Euro mwaka jana anajua kuwa ana mategemeo mamakubwa.
“Najua kwa nini nina matarajio makubwa kwa sababu ni Kombe la Dunia ndani ya Brazil, japokuwa lengo letu hilo litabaki hivyo hata kama tutakwama,” aliimbia Fifa.com.
“Mechi dhidi ya Sweden itakuwa ni ngumu: Tunajiamini na tunawaheshimu wapinzani wetu, kuliko kitu chochote. Hata hivyo tunajiamini kwamba tukwenda Brazil 2014.”
Watu wengi wanasikitika kuwa moja kati ya Ronaldo au Ibrahimovic ataikosa Brazil, lakini mshambuliaji wa PSG amesema timu yake inastahili kucheza Kombe la Dunia na watakuwepo katika upangwaji wa ratiba Desemba 6 mjini Mata de Sao Joao.
“Tuna mechi ngumu, lakini hiyo ni hali nzuri kwetu,” alisema Ibrahimoivic.
“Nimeona wachezaji wawili tofauti, wakiwa kwenye kiwango cha juu wakiwakilisha nchi zao katika hatua muhimu,” alisema Ibrahimovic.
“Kwanza haitakiwa kuifanya mechi hiyo kwa wawili hao tu, hii ni mechi kati ya Sweden dhidi ya Ureno nafikiri ikizungumza hivyo ni vizuri zaidi.”

Ukraine itawakaribisha Ufaransa walio katika hatari ya kukosa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1994 pia hawataki kurudia makosa ya 2010 yaliyotokea ndani na nje ya uwanja kilichofanya wachezaji kugomea mazoezi.
Kocha wa Ufaransa, Didier Deschamps ambaye 1998, alikuwa nahodha wa kwanza wa Ufaransa kunyanyua Kombe la Dunia wakati walipoifunga Brazil jijini Paris, amesema wachezaji wake wanachukulia kwa umakini mkubwa mchezo huo dhidi ya Ukraine.
“Wachezaji wanakuwa uwanjani, lakini ni kocha ndiye anayeongoza miguu yao,” alisema nyota huyo wa zamani Juventus.

No comments:

Post a Comment