Wednesday, 13 November 2013

Jitihada za  kumdhamini mbunge  wa  Jimbo la  Ukerewe (CHADEMA) Ndugu Salvatory Machemli zimeshindikana ikiwa ni  siku ya saba tangu awekwe mahabusu baada ya kufutiwa dhamana na Maahakama ya Wilaya ya Ukerewe.

Kaimu  Hakimu  wa mahakama  ya wilaya  ya  Ukerewe, Mrisho  Abed alisema kuwa amri hiyo  ya kwenda  rumande kwa siku 14  ilitolewa  baada  ya mshitakiwa  kushindwa  kutimiza  masharti ya dhamana. Alisema   sheria ya makosa ya  jinai  namba 20 iliyofanyiwa malekebisho mwaka 2002 kifungu cha 148 katika vifungu vidogo vya (5),(3)(C) mahakama inapewa mamlaka  ya kufuta dhamana  ya mshitakiwa.

Hakimu  Abed  alisema  chombo pekee chenye mamlaka ya kuitengua amri hiyo ni Mahakama Kuu.

Alikazia kuwasi hiyo ingekuwa chini yake, asingetoa dhamana tena kwa mshitakiwa hadi isikilizwe na kumalizika.

No comments:

Post a Comment